Wasanii mwaka 2016 uwe wa kazi na si lawama – Fella



Mkurugenzi wa kituo cha Mkubwa na Wanawe pamoja TMK Wanaume Family, Said ‘Mkubwa’ Fella, amewataka wasanii kuutumia mwaka 2016 vizuri kwa kutoa kazi nzuri na kuacha malalamiko yasiyo na tija.



Fella ambaye ametambulisha kundi jipya la muziki liitwalo Salam TMK, alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV kuwa mwaka 2016 utakuwa mwaka mwema kama wasanii watautumia vizuri.

“Ninaweza nikawaambia wasanii wajibrand vizuri, lawama ndogo ndogo hazihitajiki tena mwaka 2016,” alisema.

“Kama kuna lawama zinahitajika basi ni za jumla au ziwe lawama kama mtu kaonewa au amenyanyaswa lakini tusilalamike ilimradi kugomea vitu wakati tunajua serikali yetu imeamua mpaka kutuwekea waziri ambaye atatusikiliza na kusikiliza matatizo yetu kwa maslahi yetu. Kwahiyo tunatakiwa kuwa wamoja na tutengeneze unity nzuri ili tufikie malengo yetu kwa pamoja,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Fella ambaye pia ni diwani wa kata ya Kilungule amewataka mashabiki wa muziki kuliunga mkono kundi Salam TMK lililoachia wimbo ‘Nafsi.’

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment