Ban: Ulimwengu uwasaidie wakimbizi Syria




Maelfu ya raia wa Syria wamelazimika kuyatoroka makaazi yao
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon ametoa wito kwa mataifa yote kuonyesha umoja na wakimbizi wa Syria.

Akizungumza Geneva wakati wa kuanza mkutano wa shirika la Umoja wa mataifa la kuwashughulikia wakimbizi UNHCR, Ban amewataka mawaziri kuwatafutia makaazi takriban wakimbizi nusu milioni wa Syria kufikia mwisho mwa 2018.

Ban Ki-moon amesema ulimwengu unapaswa kushinikiza hatua madhubuti kuwasiaidia wakimbizi wa Syria.

Amesema nchi jirani na Syria, Turkey, Jordan na Lebanon zimeathirika na mzigo wa mzozo huo. Nchi zote zinaweza kuwajibika zaidi. Watoot wa Syria wanutegemea ulimwengu kuonyesha ukarimu.

UNHCR linawataka wakimbizi hao watafutiliwe makaazi, familia zijumuike pamoja na wanafunzi wamalize masomo yao ng'ambo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment