Akipiga stori na Ijumaa, Shamsa alisema mastaa kwa sasa wanagombana na kutoleana maneno machafu, kitu ambacho si kizuri kwa kazi zao kwani wote wanategemeana.
“Hiki ni kipindi cha mpito tu, mimi nawashauri mastaa wenzangu wasifikishane pabaya kisa siasa, tushindane kwa sera kupitia vyama vyetu lakini si kugombana na kutoleana maneno machafu, kesho na keshokutwa najua tutakutana tu kwenye kazi zetu tena,” alisema Shamsa.
0 comments:
Post a Comment