18:54 Mechi zamalizika
West Ham 2- 1 Chelsea
Aston Villa 1- 2 Swansea
Norwich 0-1 West Brom
Stoke 0-2 Watford
Leicester 1-0 Cyrstal Palace
18:52 Jon Obi Mikel aonyeshwa kadi ya njano kwa kumfyeka Dimitri Payet.
18:44 West Ham 2-1 Chelsea
Chelsea wafanya badiliko lao la mwisho. Baba Rahman aingia nafasi ya Cesar Azpilicueta.
18:42 BAOOOO!
Aston Villa 1-2 Swansea City
Andre Ayew afungia Swansea dakika ya 87.
18:39 West Ham 2-1 Chelsea
Radamel Falcao aingia nafasi ya Ramires. Mechi imesalia dakika nane hivi.
18:36 BAAOOOOO!
West Ham 2-1 Chelsea
Andy Carroll, aliyeingia kama nguvu mpya, aifungia West Ham.
18:34 West Ham 1-1 Chelsea
Chelsea wajiweka hatarini baada ya Asmir Begovic kutouchukua vyema mpira wa kurudishwa nyuma wa John Terry. Kipa alazimika kuutupa nje na kuwa kona. Terry aondoa kona hiyo eneo la hatari.
18:32 West Ham 1-1 Chelsea
Cheikhou Kouyate amchezea visivyo Ramires kutoka nyuma na kuonyeshwa kadi ya njano.
18:27 West Ham 1-1 Chelsea
West Ham wamtoa shujaa wao aliyewafungia bao Mauro Zarate na kumuingiza Andy Carroll.
18:26 Stoke 0-2 Watford
Almen Abdi aongezea Watford la pili.
18:23 Aston Villa 1-1 Swansea
Gylfi Sigurdsson asawazishia Swansea kupitia frikiki.
18:18 BAOOOO!
Aston Villa 1-0 Swansea
Jordan Ayew, afungia Villa bao lake la kwanza.
18:15 BAOOOOO!
Leicester 1-0 Crystal Palace
Bao lafungwa na Jamie Vardy
Vardy amejiunga na Thierry Henry, Alan Shearer, Ian Wright, Mark Stein, Emmanuel Adebayor, Ruud van Nistelrooy na Daniel Sturridge katika kufunga mabao mfululizo mechi za Ligi ya Premia. Wote walifunga mabao mechi saba mfululizo.
Van Nistelrooy ndiye mwenye rekodi kwa kufungia Man Utd bao kila mechi kwa mechi 10 mwaka 2003.
18:13 BAOOOOOO!
West Ham 1-1 Chelsea
Bao limefungwa na Gary Cahill. Amelifunga kwa kichwa baada ya kuchapwa kwa kona.
18:02 Mourinho afukuzwa uwanjani. Fabregas ameondolewa nafasi yake pakaingia Obi Mikel.
Mourinho amefukuzwa baada yake kuomba aruhusiwe kuingia chumba cha refa Jon Moss wakati wa mapumziko. Sasa anakaa na chumba cha wakurugenzi uwanjani.
18:01 BAOOOO!
Norwich 0-1 West Brom
Bao limefungwa na Salomon Rondon
18:00 Timu zote zimerejea uwanjani
17:45 Ni muda wa mapumziko sasa
Matokeo kufikia sasa
West Ham 1-0 Chelsea
Stoke 0-1 Watford
17:44 Mkasa kwa Chelsea
Nemanja Matic afukuzwa uwanjani kwa kumfanyia madhambi Diafra Sakho. Fabregas na Costa nao waonyeshwa kadi za manjano kwa kulalamika.
17:43 BAOOOO! Stoke 0-1 Watford
Bao la Troy Deeney
17:42 Cesc Fabregas atumbukiza mpira wavuni, lakini bao lakataliwa kwa kuwa alikuwa ameotea.
17: 39 BAOOOO!
Kkatika ligi ya daraja la pili, Shola Ameobi afunga bao mechi yake ya kwanza kuchezea Bolton Wanderers.
17:36 West Ham 1-0 Chelsea
Kurt Zouma akaribia sana kufunga bao kwa kichwa. Adrian na Carl Jenkinson wauzuia mpira kuvuka mstari wa goli.
17:36 Nemanja Matic aonyeshwa kadi ya njano kwa kumchezea visivyo Diafra Sakho.
17:17 BAOOOOOO!
West Ham 1-0 Chelsea
Mauro Zarate
West Ham watwaa uongozi kupitia kona. Mpira wa kichwa wa Ramires umeenda moja kwa moja kwa Mauro Zarate.
17:14 Aston Villa 0-0 Swansea
Federico Fernandez apoteza nafasi ya mwaka upande wa Swansea baada ya kona iliyopigwa na Jonjo Shelvey.
17:11 Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa anapoteza nafasi nzuri.
17:00 West Ham 0-0 Chelsea
Chelsea wanaanzisha mchezo. Uwanja umerowa kutokana na mvua ambayo imekuwa ikinyesha.
16:59 Kikosi cha Chelsea: Uwanjani: Begovic, Zouma, Cahill, Terry, Azpilicueta, Ramires, Matic, Willian, Fabregas, Hazard, Costa
Benchi: Amelia, Baba Rahman, Mikel, Loftus-Cheek, Oscar, Traore, Falcao
16:58 Kikosi cha West Ham: Uwanjani: Adrian, Jenkinson, Tomkins, Collins, Cresswell, Noble, Kouyate, Zarate, Payet, Lanzini, Sakho
Benchi: Randolph, Carroll, Valencia, Obiang, Ogbonna, Jelavic, Antonio
16.57 Klabu ya Chelsea leo imo ugenini West Ham ikijaribu kufufua kampeni yake Ligi ya Premia msimu huu baada ya kuandikisha matokeo yasiyo ya kuridhisha tangu mwanzo wa msimu.
Mechi zote za leo:
Aston Villa v Swansea 15:00
Leicester v Crystal Palace 15:00
Norwich v West Brom 15:00
Stoke v Watford 15:00
West Ham v Chelsea 15:00
Arsenal v Everton 17:30
0 comments:
Post a Comment