Fifa yakutana na wadhamini wake





Rais wa Fifa, Sepp Blatter
Shirikisho la kandanda duniani Fifa, limekutana na baadhi ya wadhamini wake wakubwa kujadili uchunguzi wa maswala ya rushwa.

Mamlaka za Marekani na Uswisi zinachunguza madai ya utoaji na upokeaji rushwa kwa viongozi wa juu wa shirikisho hilo.

Wadhamini waliokutana na shirikisho hilo ni AB InBev, Adidas, Coca-Cola, McDonald pamoja na Visa.

Ambapo shirikisho hilo la kandanda likakubaliana na wadhamini hao kufanya kazi kwa uwazi, mageuzi, na kushirikiana na washirika wake kwa ukaribu.

Katika taarifa ya pamoja ya wadhamini hao ilisema: ni matarajio yao watafanya mageuzi imara, na wataendelea kushirikana na Fifa.".
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment