Mwanamitindo Hamisa Mobeto amesikitishwa na Tanzania kuendelea kuwa nchi isiyojiweza kiviwanda licha ya kuwa na rasilimali na nguvu kazi ya kutosha.
Akizungumza jana kwenye ukumbi wa New Africa Hotel katika mdahalo uliopewa jina ‘Ndoto Kubwa’ ulioandaliwa na Tanzania Initiative kwendana na kilele cha siku ya vijana duniani, Mobeto alisema anachukizwa na wasichana kutegemea urembo kutoka China, Marekani na nchi zingine.
“Inasikitisha mimi kila kitu ninachovaa nguo kutoka nchini nyingine, ili nionekane lazima nivae nywele kama mchina, nivae nguo kama mmarekani, viatu sijui kama mtu gani,” alisema Mobeto.
“Sisi tunaamini Tanzania tuna maeneo mengi sana ambayo hayajatumika. Serikali ina uwezo wa kujenga kiwanda cha kutengeneza nguo, ambapo sisi kama sisi tunaweza kuvaa vitu ambavyo vinatoka kwetu, ambapo tuwe proud kwamba nchi yetu tunavaa vazi letu hili linatoka Tanzania,” aliongeza.
“Inasikitisha sana kuona mmasai amekaa Magomeni sehemu fulani barabarani anatengeneza viatu vya kimasai lakini nchina amekuja anatengeneza hivyo hivyo viatu vya kichina ambavyo ni fake na watanzania wanavinunua na kuvivaa wakati tungeweza kumwezesha yule mmasai wetu ambaye amekaa chini na kupigwa na jua kwa kutengeza bidhaa bora.”
Akizungumza jana kwenye ukumbi wa New Africa Hotel katika mdahalo uliopewa jina ‘Ndoto Kubwa’ ulioandaliwa na Tanzania Initiative kwendana na kilele cha siku ya vijana duniani, Mobeto alisema anachukizwa na wasichana kutegemea urembo kutoka China, Marekani na nchi zingine.
“Inasikitisha mimi kila kitu ninachovaa nguo kutoka nchini nyingine, ili nionekane lazima nivae nywele kama mchina, nivae nguo kama mmarekani, viatu sijui kama mtu gani,” alisema Mobeto.
“Sisi tunaamini Tanzania tuna maeneo mengi sana ambayo hayajatumika. Serikali ina uwezo wa kujenga kiwanda cha kutengeneza nguo, ambapo sisi kama sisi tunaweza kuvaa vitu ambavyo vinatoka kwetu, ambapo tuwe proud kwamba nchi yetu tunavaa vazi letu hili linatoka Tanzania,” aliongeza.
“Inasikitisha sana kuona mmasai amekaa Magomeni sehemu fulani barabarani anatengeneza viatu vya kimasai lakini nchina amekuja anatengeneza hivyo hivyo viatu vya kichina ambavyo ni fake na watanzania wanavinunua na kuvivaa wakati tungeweza kumwezesha yule mmasai wetu ambaye amekaa chini na kupigwa na jua kwa kutengeza bidhaa bora.”
0 comments:
Post a Comment