Mama Diamond Platnumz Amfunika Zari kwa Mbizi Kwenye Bwawa la Kuogelea




MAMA’KE Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ameonesha umahiri mkubwa wa kuogelea kiasi cha kumfunika mkwe wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwenye bwawa la kuogelea lililopo nyumbani kwa Diamond, Tegeta-Mivumoni jijini Dar.

Mama huyo alionekana akipiga mbizi na mtoto wake Esma, huku akionyesha manjonjo ya kuogelea kwa kasi tofauti na Zari anavyoogelea katika bwawa hilo.

“Bi mkubwa yuko vizuri sasa maana anapiga mbizi siyo mchezo kabisa hata Zari haoni ndani, spidi yake ni kali kuliko Zari,” alisema mwanafamilia mmoja ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini huku akimtumia mwandishi wetu picha za mama Diamond akiogelea.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment