Manchester United yaicharanga Club Brugge ya Ubelgiji 3-1


Manchester United imeanza vizuri mchezo wa kwanza wa mchujo kuwania nafasi kuingia hatua ya makundi ya michunao ya klabu bingwa barani ulaya,

Baada ya kupata ushindi wa 3-1 dhidi ya Club Brugge ya Ubelgiji . Brugge ilipata bao lao mapema dakika ya 8 ya mchezo baada ya kiungo wa Man U Michael Carrick kujifunga.


Mshambuliaji mpya wa kikosi hicho cha mashetani wekundu Memphis Depay akasawazisha bao hilo dakika ya 14 kabla ya kuongeza bao la pili dakika 43, kiungo aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Wayne Rooney, Mbelgiji Marouane Fellaini, akifunga bao la tatu lilihitimisha ushindi huo.

Matokeo mengine ya michezo ya mchujo kuwania kuingia hatua ya makundi ya klabu bingwa ulaya ni:
Astana 1 APOEL Nicosia 0
BATE Borisov 1 Partizan Belgrade 0
Lazio 1 Bayer Leverkusen 0
Sporting CP 2 CSKA Moscow 1
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment