Couple ya waigizaji, Angelina Jolie na mumewe Brad Pitt wanatarajia kuongeza member mpya kwenye familia yao yenye watoto 6.
Kwa mujibu wa Radar Online, couple hiyo inasemekana wanatarajia kuasili mtoto wa 7 kutoka Syria.
Chanzo kimoja kimesema kuwa kwasasa wako kwenye taratibu za mwisho za kumuasili mtoto huyo yatima ambaye Jolie alikutana naye alipotembelea vituo vya wakimbizi nchini Syria.
Watoto sita wa couple hiyo ya Hollywood ni Maddox (13), Pax (11), Zahara (10), Shiloh (8) na mapacha Vivienne na Knox wote wana umri wa miaka 6.
0 comments:
Post a Comment