Bonge la Nyau aeleza jinsi jina lake lilivyomuumbua mbele ya mama yake na Matonya

Mama wa msanii wa muziki, Matonya amesababisha rapper wa rapper wa ‘Vice Verse’ Bonge la Nyau, kuupa uzito uamuzi wa kubadilisha jina lake na kuwa Nyauloso.

Bonge la nyau

Bonge la Nyau amesema mama yake Matonya alishtuka baada ya kutambulishwa kwake mara ya kwanza.
“Nilikuwa naitwa Bonge la Nyau lakini sasa hivi Nyauloso,” aliimbia 255 ya XXL kwenye Clouds FM.
“Nimejiita Bonge la Nyau mimi lakini watu wengine hawapendi, wananiambia jina baya na mwonekano ni tofauti na jina. Juzi nilienda nyumbani kwa akina Matonya walitualika chakula, baada ya kumaliza chakula tukaanza kutambulishwa, wametambulishwa wengine baada ya kufika kwangu, akatambulisha ‘mama huyu anaitwa Bonge la Nyau’, akashtuka, akaanza kucheka! Akaniuliza ‘umefikiria nini mwanangu mpaka kujiita hivyo’, nikagundua ni kitu fulani kina sound kinatisha zaidi. Lakini sasa baada ya kujiita Nyauloso kila mtu amefurahia.”


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment