Jux adai hawezi kufanya show za kampeni za kisiasa


Mwimbaji wa muziki wa R&B, Jux amesema hawezi kufanya show za kampeni za kisiasa kwa kuogopa kuwachanganya mashabiki wake.



Akizungumza na kipindi cha Planet Bongo cha EATV, Jux alisema akipanda kwenye majukwaa ya siasa itakuwa ni kama anawashinikiza mashabiki wake kuchagua viongozi wasiowataka.

“Watanzania tulivyo, mimi kama kuna mtu ananipenda mpaka akaamua kuchora Jux au akaandika Jux kwenye mwili wake, mtu huyo nina nguvu ya kumshawishi na akafanya kitu bila ya yeye kutaka,” alisema.

“Kwahiyo leo nikisimama kwenye stage nikasema tumchague mtu fulani, kuna watu wengi sana katika akili zao watasema hata Jux mwenyewe kamchagua mtu fulani. Ndio maana hata viongozi wa siasa kwenye kampeni zao wanachagua wasanii ili kushawishi. Kwahiyo mimi naomba kama shabiki wangu uniangalia, mimi mwenyewe ni siri yangu, kuna kiongozi ambaye namuamini. Lakini wewe angalia mwenyewe, nenda Chadema au CCM. Msikilize Magufuli au Lowassa, wewe si una akili?”

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment