Picha: Mastaa wa muziki wa Afrika Davido, AKA na Diamond wakionesha mapenzi mazito kwa watoto wao wa kike
Mastaa wa muziki wa Afrika Diamond wa Tanzania, Davido wa Nigeria na rapper AKA wa Afrika Kusini wameshare picha za kudhihirisha ni jinsi gani wanajivunia kuwa ‘baba’. Mastaa hao wote watoto wana watoto wa kike.
Rapper AKA ambaye hivi karibuni ametengana na mama wa Mwanaye DJ Zinhle ameshare picha akiwa amembeba mtoto wake kwa hisia na kuandika “Real stuff.“
Davido alishare picha ya mtoto wake na kuandika “AURORA DABBIN ON EM!! #BILLIONAIREBABY”.
Diamond Platnumz ambaye amekuwa akionesha mapenzi mazito kwa binti yake Tiffah toka amezaliwa, ameshare picha mpya akiwa amempakata mwanaye ikiwa ni siku chache kabla ya tarehe ya kumuonesha sura kwa mara ya kwanza Septemba 20.
0 comments:
Post a Comment