Mwezi uliopita Rais wa Zimbabwe
Robert Mugabe alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya wabunge wa vyama
vya upinzani kumzomea wakati akitoa hutuba wakimshutumu kushindwa
kuiongoza vyema nchi yao.
Headlines zimerudi tena kwa Rais
huyo baada ya jana Bunge hilo kuahirisha matangazo ya LIVE ya redio na
Televisheni ya hotuba ya Mugabe kutoka kwa vyama vya upinzania kutishia
kuvuruga hotuba hiyo kwa mara nyingine.
Wapinzania hao wamekua wakimlaumu
rais wao kuendelea kung’ang’ania madarakani wakati uchumi wa nchi hiyo
ukiendelea kudidimia kila siku.
Rais Mugabe ambaye sasa ametimiza miaka 91 amekuwa madarakani tangu mwaka 1980.Spika wa Bunge Jacob Mudenda amevionya vyama hivyo kuacha mara moja vurugu hizo lakini ziligonga mwamba na vituo vya matangazo kusitisha kurusha matangazo hayo LIVE.
0 comments:
Post a Comment