Ukame wawaathiri watu 250,000 Somaliland



Ukame

Mashirika ya misaada yanasema watu robo ya milioni wanaathirika kutokana na ukame katika eneo lililojitangazia uhuru la Somaliland.

Mashirika hayo yanasema utapia mlo umeathiri watu vibaya hasa watoto wa chini ya miaka mitano. Watu kumi na watatu wameripotiwa kufa.

Kulingana na mashirika hayo asilimia arobaini ya mifugo imekufa kutokana na ukosefu wa maji na uhaba wa chakula.

Familia zinalazimika kuishi bila vyakula vya kutosha , kunywa maji machafu na kuhamahama kutafuta chakula.

Maeneo yalioathirika zaidi ni yale ambayo huzalisha chakula kwa kiwango kikubwa.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment