Klabu ya TP Mazembe ya Congo DRC, imefanikiwa kuingia hatua ya fainali ya klabu bingwa barani Afrika na itakutana na klabu ya Algeria USM Alger.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta jana alifanikiwa kupiga mabao mawili na uwanja mzima ulikuwa ukimshangilia kwa kuimba jina la mchezaji huyo. Naye Roger Assale alifunga goli moja na kuipa TP Mazembe ushindi wa magoli 3-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani jijini Lubumbashi dhidi ya El Merreikh kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali.
0 comments:
Post a Comment