Linah adai anatamani kutoka kimapenzi na Wizkid


Msanii wa muziki Linah Sanga ameweka wazi kwamba anatamani kutoka kimapenzi na staa wa muziki kutoka Nigeria Wizkid.


Akizungumza katika kipindi cha Enewz cha East Africa Television Jumanne hii, Linah amesema mwanaume ambaye anawish kuwa naye ni Wizkid.

“Msanii gani wa Afrika wakiume ambaye ningependa kuwa na mahusiano naye ambaye nilikuwa nampenda au nawish kuwa naye ni Wizkid,” alisema Linah.

Pia Linah amedai hakupendezwa na tetesi ambazo zilizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa alilala na Wizkid wakati ambapo alikuwa Nigeria kwa ajili ya show.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment