Nay wa Mitego hajui nguzo za hip hop – Kimbunga


Rapper Kimbunga Mchawi amesema kuwa Nay wa Mitego hajui muziki na wala hajui nguzo za hip hop.



Kimbunga amesema hayo alipohojiwa na kwenye kipindi cha Enews kinachorushwa na East Africa Television.

“Msanii Nay wa Mitego sio msanii mkali, hajui nguzo za hip hop, hajui muziki hata aimbe wimbo gani hawezi, na siwezi kumshirikisha na sijawahi kushirikiana naye, yeye ndo aliwahi kunishirikisha kwenye nyimbo zake, na kwasababu kulikuwa na wasanii wengine kama kina Baghdad, nikaona kazi nzuri nami nikakubali”, alisema Kimbunga.

Wasanii hao wawili wamekuwa na bifu kwa miaka kadhaa sasa.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment