Nick wa Pili akanusha kumwandikia Joh Makini mashairi



Joh Makini aliongelea issue kuwa kuna watu wanadhani yeye huandikiwa mashairi na mdogo wake Nick wa Pili kwenye ngoma yake Don’t Bother.



Na sasa Nick amezungumzia jambo hilo analolielezea kama ni propaganda. Amesema Joh alianza kuhit na nyimbo kibao kama Chochote Popote na album ya Zamu Yangu kipindi ambacho hakuna alikuwa akimfahamu yeye na alikuwa hawezi kuandika kama kaka yake.

“Sijui ni nani alianzisha hiyo propaganda, ni kama hiyo propaganda ya kuwa Weusi wanabebwa. Ni rahisi sana kusema Weusi wanabebwa, ni ngumu sana kusema Don’t Bother wanabebwa, ngumu kusema Baba Swalehe anabebwa lakini unaposema Weusi unakuwa unabebwa ukweli,” Nick aliiambia 255 ya XXL kupitia Clouds FM.



“Joh Makini anajiandikia mwenyewe lakini sisi kama Weusi tukiwa studio tunasaidiana mashairi hilo liko wazi, nilishasaidiwa sana, kila mtu alishawahi kusaidiwa sana, hauwezi kuwa unajua kila kitu,” amesisitiza Nick.

Credit bongo5

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment