Ripoti: Tiwa Savage asainishwa na Roc Nation


Jay Z ameripotiwa kukubali kusainishwa kwa msanii wa Nigeria, Tiwa Savage kwenye label yake, Roc Nation.



Kwa mujibu wa ripoti ya Urban View ya Nigeria, Jay Z ameshawishiwa na uwezo wa Tiwa na alikubali kusainiwa kwake May 24. Imedaiwa kuwa deal lilisimamiwa na wawakilishiwa Roc Nation, Briant Biggs na Shawn Pecas.

Hafla rasmi ya kumtangaza kama mwana familia mpya wa Roc Nation haijafanyika na bado label hiyo haijathibitisha. Kama ni kweli, Tiwa atakuwa msanii wa kwanza kutoka Nigeria kusainishwa kwenye label hiyo na kujiunga na Rihanna, Big Sean, DJ Khaled na wengine.

Balozi huyo wa Forte Oil, MTN na Pepsi kwa sasa yupo chini ya label ya Don Jazzy, Mavin Records.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment