Wolper adai kuna filamu inakuja akiwa na Diamond



Jacqueline Wolper anaweza kuwa kimya kwenye filamu kwa kipindi kirefu lakini ana mipango mikubwa kwenye tasnia hiyo.



Muigizaji huyo amedai kuwa na mpango wa kuja na filamu aliyoshirikiana na ex wake Diamond Platnumz. Wolper ambaye kwa sasa ni mpenzi wake na Harmonize, alikiambia kipindi cha Take One cha Clouds TV wiki hii kuwa pamoja na kwamba aliwahi kuwa na uhusiano na staa huyo na kisha kuachana, bado wamebaki kuwa washkaji wa nguvu.

Alisema ukaribu wao ni zaidi ya urafiki na wameendelea kushirikiana katika mengi. Ni kweli kwakuwa Wolper ndiye ex wa Diamond pekee aliyeonekana kwenye video ya Utanipenda.

Hata hivyo hakusema ni lini filamu hiyo itaanza kufanyiwa maandalizi. Kama itakuwepo, hiyo itakuwa filamu ya kwanza ya Diamond.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment