Barnaba: Nimeifumua upya album niliyopanga kuitoa ili kuipa nguvu zaidi


Barnaba amedai kuwa amelazimika kuifumua upya album yake aliyokuwa amepanga kuitoa mwaka jana ili kuipa nguvu zaidi.



Mwaka jana, muimbaji huyo aliahidi kuitoa album yake aliyokuwa ameipa jina ‘Nane Nane’ kwenye siku wa Wakulima (August 8) lakini aliahirisha baada ya sponsor aliyekuwa ameingia ubia kwenye album hiyo kubadilisha mawazo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Loudspika cha Africa Swahili FM, Morogoro, Barbaba amedai kuwa ushindani toka kwa wasanii wapya ni sababu za kujipanga upya.



“Vitu vingi nimebadili, kuna changamoto nyingi, majanki wanafanya vizuri sana, ukiruka huku unakutana na mashine kwahiyo inabidi kuwa makini. Na mimi nikiwa kama mtu mzima, nafasi hizi za kuwa kwenye ubora nazihitaji, so I have to do something beautiful,” amesema Barnaba.
Barnaba amedai kuwa siku ya Valentine’s atatoa bonus track ambayo huenda ikabeba jina la album hiyo. Juu ni interview nzima aliyofanya na mtangazaji Ergon Elly.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment