Jim Jones amaliza bifu lake na Jay Z, asaini mkataba na Roc Nation
Mafahari wawili wa muziki wa hip hop kutoka Marekani, Jay Z na Jim Jones wamemaliza bifu lao lililodumu takribani miaka 13.
Chanzo kimoja kimeuambia mtandao wa TMZ pia Jim amesaini mkataba na lebo ya Roc Nation inayomilikiwa na Jay Z.
Mmoja wa watu wa lebo hiyo, Vic Mediana ameweka picha kwenye mtandao wake wa Instagram inayomuonyesha rapper huyo alisaini mikataba ya leebo hiyo na kuandika, “It’s a done deal… Jim Jones/Roc Nation. #rocnation #vamplife.”
0 comments:
Post a Comment