‘Game’ ya Navy Kenzo ft. Vanessa Mdee yakamata namba 1 kwenye Top 10 ya The Beat Fm ya Nigeria


Kundi la Navy Kenzo limeanza kuyaona matunda ya kufanya kazi na Vanessa Mdee ambaye tayari amejitengenezea connection nyingi nchini Nigeria na Afrika kwa ujumla.

game2
Baada ya kuchia video kali iliyoongozwa na director wa Afrika Kusini, Justin Campos wimbo wao ‘Game’ ambao wamemshirikisha Vanessa, tayari umeanza kufanya vizuri kwenye chati za muziki za vituo vya Nigeria.
Wiki hii (August 21) wimbo huo umekamata namba 1 kwenye African Top 10 ya kituo kikubwa cha Radio cha Nigeria, The Beat 99.9Fm.
GAMEno1
Mtanzania mwingine ambaye yumo kwenye chati ya wiki hii ya kituo hicho ni Alikiba, ambaye wimbo wake ‘Chekecha Cheketua’ umekamata nafasi ya 9.
African Top 10 huwa inasikika kila Ijumaa kupitia kipindi cha Morning Rush cha The Beat 99.9 Fm ya Lagos, Nigeria.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment