Usiseme hatuna hela, sema huna hela!
Katika kuhakikisha tabasamu kwenye uso wa mrembo wake Kylie Jenner halikauki, rapper Tyga amemsurprise kwa kumnunulia gari aina ya Ferrari 482 Italia yenye thamani ya $320,000 ambazo ni zawadi ya shilingi milioni 665!
Kylie Jenner ametimiza umri wa miaka 18 Jumatatu hii.
Kwa mujibu wa mtandao wa People, Tyga alimpa mpenzi wake gari hilo lenye rangi nyeupe kwenye sherehe iliyofanyika huko West Hollywood iliyohudhuriwa na mastaa kibao.
Mastaa waliohudhuria sherehe hiyo ni pamoja na Kim Kardashian, Kanye West, Khloe, Kourtney, Kendall, Kris na Caitlyn Jenner.
0 comments:
Post a Comment