Sadio Mane kuelekea Man Utd





Sadio Mane

Klabu ya Southampton ya Uingereza imakubali kuwa Manchester United wanavutiwa na wana mpango wa kumsajili winga kutoka nchini Senegal Sadio Mane. Ieleweke kwamba, United ilifanya jitihada kumapata mchezaji huyo mwenye miaka 23 tokea juma lililopita lakini Southampton wamekanusha kupokea ofa yoyote.

Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21.

Mane alifunga magoli 10 katika michezo 32 aliyocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu (hat-trick) kwa muda mfupi zaidi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment