Uchaguzi wa Haiti wafanyika miaka 4 baadaye
Wananchi wa Haiti wanashiriki kwenye uchaguzi wa wabunge leo.
Uchaguzi huu uliahirishwa miaka minne iliyopita.
Wagombea zaidi ya 1,800 , kutoka vyama vingi vya kisiasa , wanawania viti vya ubunge.
Bunge la taifa mjini Port-au-Prince, lilifutwa mwezi wa Januari
Uchaguzi huo unaonekana kama ishara ya utulivu katika nchi hiyo maskini.
Bunge la taifa mjini Port-au-Prince, lilifutwa mwezi wa Januari, kwa sababu ya kushindwa kufanya uchaguzi.
Tangu wakati huo Rais Michel Martelly ameongoza nchi hiyo kwa amri yake.
Rais mpya atachaguliwa mwezi Oktoba.
Bwana Martelly mwenyewe haruhusiwi kushiriki uchaguzi huo
0 comments:
Post a Comment