Msanii huyo ambaye ni mdogo wake na Ali Kiba, ameiambia Bongo5 hivi karibuni kuwa lengo lake ni kuhakikisha na yeye anafanya vizuri kimataifa.
“Tayari nimeanza mazungumzo ya kolabo na wasanii wa Nigeria ili kutanua wigo wangu wa muziki,” amesema. “Kila kitu hapa ninapozungumza kinaenda vizuri, siwezi kuwataja ni akina nani lakini nimezungumza nao. Ni wasanii wakubwa na nikifanya nao kazi zitakuwa na impact katika muziki wangu. Tayari nimeshawatumia kazi nasubiria wapokee audio zangu ili tujue ni lini kazi zinaanza,” ameongeza.
Kiba ameeleza kuwa kufanya kolabo na wasanii wa Nigeria kuna faida kwakuwa ni wasanii ambao muziki wao unafanya vizuri katika kila kona ya Afrika kwa sasa.
0 comments:
Post a Comment