Mafanikio ya Nana aliyoshirikishwa na Diamond Platnumz yamemfanya msanii wa Nigeria, Flavour naye kumshirikisha staa huyo wa Tanzania.
Tangu itoke miezi minne iliyopita video ya Nana imefikisha zaidi ya views milioni 4.7 kwenye Youtube na tayari inawania tuzo kadhaa za kimataifa.
Flavour aliiambia website ya DSTV kuwa wimbo aliomshirikisha Diamond utatoka siku za usoni. Flavour alisema ameamua kumshirikisha Diamond baada ya kuona ukubwa wake Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa Diamond ameonesha kuwa ni mchapakazi na ‘down to earth’ na anaamini kazi yao mpya itahit pia.
0 comments:
Post a Comment