KUBENEA Amlipua na Kumuumbua Vibaya Dr Slaa Mkutanoni Kyela Mbeya



1. Amesimulia sakata zima la Richmond kwa kudai kuwa wakati likiwakilishwa bungeni kulikuwa na ripoti mbili. Moja ya kumchafua Lowassa na ya pili ikidai Kikwete ndo mhusika wa Richmond
Amesema aliyekuwa akipinga ujio wa Lowassa Chadema ni Baregu na siyo Dr Slaa.

2. Amesema kamati kuu ya chadema ilijiridhisha kuwa Dr Slaa asingeweza kushinda uchaguzi wa mwaka huu kama angesimamishwa kuwa mgombea wa urais

3. Amedai kilichomponza Slaa ni mkewe ambaye alikuwa na uchu wa kuwa first lady

4. Baada ya hapo,Slaa alianza kampeni za kumpinga Lowassa ili ateuliwe yeye. Alimtuma Sugu aende Mbeya akawaambie waumini wa makanisa yote kuwa wao wanamtaka Slaa na sio Lowassa, lkn Sugu Alikataa.

5. Slaa pia alijaribu kumrubuni Tundu Lissu atangaze kumpinga Lowassa lakini naye alikataa pia na kujikuta akibaki peke yake, hali iliyomfanya ajivue uanachana

6. Amesema Slaa alikuwa Padri akaasi,alikuwa na mke akaasi, alikuwa CCM akajitoa, je ana principle gani za kuwashawishi watanzania wamuamini?
Dr Slaa ni msaliti na anatumia umaarufu wake vibaya

7. Slaa anadai kuwa nyaraka za Richmond alipewa na Mwakyembe, lakini ukweli ni kuwa mwakenye hawezi kuwa mtu sahihi wa kutoa nyaraka za Richmond kwa sababu wakati wa Ripoti hiyo, Mwakyembe alikuwa na kampuni yake ya kufua umeme ambayo alitaka ipite. Baada ya kukwama ndo akaanza ugomvi na Lowassa


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment