Luke aliumua kwenye mchezo wa jana wa ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya wenyeji PSV nchini Uholanzi. Katika mchezo huo United ililala 2-1. Shaw alimwaga machozi wakati anatolewa nje kutokana na uchungu wa maumivu makali.
Alipatiwa huduma ya kwanza hapo hapo uwanjani na aliwekewa hewa ya ziada mjini Eindhoven kabla ya kukimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi.
Luke atarejeshwa Manchester ambako anatarajiwa kufanyiwa upasuaji.
0 comments:
Post a Comment