Maneno ya mimi kumzidi umri Iyobo yananiumiza sana kwa kweli – Aunty Ezekiel

aunty

Aunty amesema kuwa anashangazwa na watu wanaomsema kuhusu kumzidi umri Iyobo, kitu ambacho kwake hakimsumbui.

“Kwani wakati tunatongozana hatukujua kuwa tunazidiana umri? Mbona watu wanashindwa kufanya mambo ya msingi na kukalia majungu?” aliuliza Aunty alipohojiwa na Global Publishers.
Ameahidi kulinda uhusiano wake na Iyobo ambaye ni miongoni mwa dancers wa Diamond licha ya kuandamwa na maneno.

“Kwetu sisi suala la umri ni namba tu, labda nikuulize, ulishaona mtoto anambebesha mwanamke mimba? Maneno ya mimi kumzidi umri Iyobo yananiumiza sana kwa kweli, lakini nitaulinda uhusiano huu hadi mwisho,” alisema Aunt Ezekiel.
Chanzo: GPL


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment