Sio kitu cha ajabu kwakuwa waliamua kufanya mapumziko yao kuwa ‘private’ zaidi lakini kupitia picha walizopost watu waliweza kugundua.
John alipost picha mbili akiwa visiwani humo ambapo moja mke wake Chrissy anaonekana akimbusu shavuni na nyuma ikionekana minazi ya Zanzibar.
Katika picha hiyo John aliandika tu, “Vacation has begun.”
Katika picha nyingine ambayo inaonesha wazi mandhari ya Zenji, muimbaji huyo aliandika: Vacation vibes.”
Picha zinaonesha kuwa wawili walikaa Zanzibar kwa siku mbili au tatu tu.
Wawili hao walienda Zanzibar wakati huo tamasha la ZIFF lilikuwa limefunguliwa. Hii ni mara ya pili muimbaji huyo kwenda Zanzibar. Mwaka 2009 alishoot video ya wimbo wake Show Me huko.
0 comments:
Post a Comment