Ujue Ukweli wa Edward Lowassa Kukimbia Midahalo ya Urais




Lowassa na Magufuli

Vyama vyote vya siasa vimekubali kufanya mdahalo wa wagombea wa Urais kwenye vyombo vya habari lakini vyama vinavyounda UKAWA vimekataa kushiriki kwenye midahalo hiyo kwa kutoa sharti moja la kutomshirikisha mgombea wao na badala yake waende wenyeviti wa vyama.

Utaratibu wa dunia nzima kwenye midahalo wanahudhuria wagombea na siyo wenye viti wa vyama... Yaani Rais Kikwete aache majukumu yake ikulu halafu aende kwenye vyombo vya habari kufanya midahalo wakati kwenye midahalo wanazungumzia sera za chama husika na sasa aliyebeba sera za CCM ni Ndugu Magufuli.

Baada ya kufanya uchunguzi sababu zifuatazo zimebainika kuwa ndiyo vigezo vya kumfanya mgombea wa UKAWA ndugu Lowassa kususia midahalo hiyo
1. Afya yake ni dhaifu na haimruhusu kukaa muda mrefu bila kupewa dawa ya kumuongezea nguvu. kwenye mikutano yake ya kampeni hajawahi kuzungumza zaidi ya dakika 15, sasa atawezaje kuhudhuria mdahalo akaongea zaidi ya nusu saa?

2. Amehusika sana kwenye kashfa nyingi za ubadhilifu wa mali za umma na hana uwezo wa kukataa ukweli huo, hata alipoulizwa na waandishi wa habari huko Dodoma alikataa kulijibu hilo swali, na endapo atahudhuria kwenye mdahalo wowote hilo swali hawezi kuliepuka

3. Chama chake hakina sera nzuri, anakosa kitu cha kuongea awapo mbele ya watu kwakua chama chake hakijaandaa ilani nzuri yenye sera za kumkomboa Mtanzania. Wakati wenzake wanatoa sera za kupunguza gharama za ujenzi yeye anamwaga sera za kuwatoa jela akina Babu Seya na kubomoa nyumba za nyasi nchi nzima kwa muda wa siku 100

By Aisha Idd
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment