Rais wa Iran Hassan Rouhani na kiongozi kutoka Saudi Arabia
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ameomba mataifa ya Saudi Arabia na Iran kumaliza mozozo wa sasa wa kidiplomasia kati yao.
Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje amesema kwamba Bwana Kerry amewasiliana kwa njiya ya simu na Mawaziri wa mambo ya nje kutoka pande mbili. Saudi Arabia ilikatiza uhusiano wa kidiplomasia na Iran baada ya waandamanaji kushambulia ubalozi wa Saudia mjini Tehran.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ameomba mataifa ya Saudi Arabia na Iran kumaliza mozozo wa sasa wa kidiplomasia kati yao.
Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje amesema kwamba Bwana Kerry amewasiliana kwa njiya ya simu na Mawaziri wa mambo ya nje kutoka pande mbili. Saudi Arabia ilikatiza uhusiano wa kidiplomasia na Iran baada ya waandamanaji kushambulia ubalozi wa Saudia mjini Tehran.
Kumekua na maandamano kulaani kunyongwa kwa kiongozi wa Kiongozi wa Kishia Nimr Al-Nimr
Kumekuwa na misururu ya maandamano kulaani kunyongwa kwa kiongozi wa madhehebu ya Kishia nchini Saudia.
Iran inayofuata madhehebu ya Kishia na Saudi Arabia inayofuata madhehebu ya Kisunni zimekua zikikabiliana katika vita vinavyokumba mataifa ya Yemen na Syria.
Baraza la Usalama limekosoa vikali kulengwa kwa ubalozi wa Saudia huko Tehran lakini taarifa hiyo haikugusia kunyongwa na kiongozi wa kishia Sheikh Nimr al-Nimr na watu wengine waliopatikana na hatia ya ugaidi.
Kumekuwa na misururu ya maandamano kulaani kunyongwa kwa kiongozi wa madhehebu ya Kishia nchini Saudia.
Iran inayofuata madhehebu ya Kishia na Saudi Arabia inayofuata madhehebu ya Kisunni zimekua zikikabiliana katika vita vinavyokumba mataifa ya Yemen na Syria.
Baraza la Usalama limekosoa vikali kulengwa kwa ubalozi wa Saudia huko Tehran lakini taarifa hiyo haikugusia kunyongwa na kiongozi wa kishia Sheikh Nimr al-Nimr na watu wengine waliopatikana na hatia ya ugaidi.
0 comments:
Post a Comment