Shein atangazwa kuwa Rais wa Zanzibar, apata ushindi wa asilimia 91.4


Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jecha Salim Jecha amemtangaza Dr. Mohammed Shein kuwa Rais wa Zanzibar kwenye uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, 2016 kwa asilimia 91.4.



Kwa mujibu wa Jecha, Shein amepata ushindi wa kishindo wa kura 299,982 ambazo ni sawa na asilimia 91.4. Nafasi ya pili imeshikiliwa na mgombea urais wa ADC, Hamad Rashid aliyepata kura 6,734 huku Maalim Seif Sharif Hamad (CUF) akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 6,076.

Kutokana na matokeo hayo, Dk. Ali Mohamed Shein ndiye atakayeendelea kuiongoza Zanzibar kwa muhula wake wa mwisho kwa mujibu wa Katiba.

Hatua hiyo imekuja baada ya kujitokeza dosari katika uchaguzi mkuu wa mwezi oktoba mwaka jana na kuamriwa uchaguzi huo kurudiwa.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment