Msanii wa muziki kutoka TMK Wanume Family, Chege Chigunda baada ya kufanya vizuri na wimbo wake ‘Sweety Sweety’ aliyomshirikisha Runtown, anatarajia kuweka kambi nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya kazi yake mpya.

Akizungumza na Jumatatu hii, Chege amesema kazi hiyo itatoka katikati ya mwezi wa Ramadhani.
“Katika kati ya mwezi ujao nasafiri kwenda Afrika Kusini kushoot video ya wimbo wangu mpya, ni kolabo. Siwezi weka wazi nimefanya na nani lakini ni kazi kali, yaani mwendo bandika bandua,” alisema Chege.
Chege alisema kazi hiyo inatarajia kutoka katikati ya mwezi wa Ramadhani.
0 comments:
Post a Comment