Diamond Platnumz anaitumia vizuri ziara yake ya Ulaya. Akiwa jijini Paris, Ufaransa alitembelewa na msanii mkongwe wa Congo, Awilo Longomba ambaye kumbe ni rafiki yake wa muda mrefu na Zari anayelielezea kutano lao kwa maneno ‘My good friend @awilolongomba came to visit, hope you do some business with hubby. Was great seeing you.’

Hajaishia hapo – ameingia studio na Fally Ipupa aliyeiwekea maneno picha aliyoweka Instagram, ‘Music doesn’t sleep…with my Brother @diamondplatnumz.”
Kwa wasanii dakika chache za kukutana studio kinaweza kuzalisha hit kubwa.
Katika hatua nyingine Diamond amewahi kuonekana akiimba wimbo wa 2face Idibia, African Queen mara kibao.
Aliwahi kuuimba pia kwenye msimu wa pili wa Coke Studio Africa na kwa namna anavyouimba ni rahisi kugundua kuwa Mnigeria huyo amemuinspire kwa kiasi kikubwa.
Hivyo muimbaji huyo wa ‘Utanipenda’ ameamua kumpa heshima msanii huyo anayejiita 2 Baba kwa sasa kwa kuweka picha yake kwenye profile yake Instagram yenye followers zaidi ya milioni mbili sasa.

Ni njia nzuri ya kutoa heshima kwa wakongwe na hiyo inamweka karibu nao – strategy!
0 comments:
Post a Comment