Hawa ni washambuliaji 7 wanaomuumiza kichwa Hodgson kwenda UERO 2016



Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson anaelekea kuwa na wakati mgumu kuchagua washambuliaji watakaoisaidia timu hiyo kwenye michuano ya Uero mwaka huu nchini Ufaransa.



Mpaka sasa Hodgson ana chaguo la wachezaji saba ambapo anatakiwa achague wachezaji wanne au watano kati yao.

Hawa ni washambuliaji wanaomuumiza kichwa Hodgson kufanya uchaguzi yupi atakayeshiriki michuano ya Uero 2016.

Harry Kane



Kane ndiyo mchezaji anayeongoza kwa ufungaji kwenye ligi ya Uingereza akiwa ameshafunga magoli 24. Mpaka sasa anaonekana kuingia kwenye orodha ya wachezaji wanaoweza wateuliwa na Hodgson kwenye timu ya Uingereza kushiriki michuano ya Uero.

Games 34

Games started 34

Mins played 3,008

Assists 1

Goals 24

Chances created 41

Goals/game 0.71

Win rate 56%

Jamie Vardy



Nyota huyu amesaidia Leicester City kushika usukani wa kuongoza ligi ya Uingereza kwa pointi 73. Vardy ameshafanikiwa kufunga magoli 22 akishika nafasi ya pili nyuma ya Harry Kane wa Tottenham.

Games 34

Games started 34

Mins played 2,959

Assists 6

Goals 22

Chances created 47

Goals/game 0.65

Win rate 62%

Wayne Rooney



Rooney ndiye nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza na tayari anashikilia rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote kwenye timu ya taifa akifunga magoli 51. Japo kwa msimu huu anaonekana kutofanya vizuri sana kwenye timu yake ya Manchester United na majeraha yaliyomuandama ambayo yalimfanya kukaa nje ya uwanja kwa muda kidogo.

Games 23

Games started 22

Mins played 1,972

Assists 4

Goals 7

Chances created 34

Goals/game 0.30

Win rate 44%

Daniel Sturridge



Japo kipindi cha nyuma alionekana kutofanya vizuri kwenye timu ya Liverpool, Sturridge kwa sasa ameonekana kuwa ni mmoja wa washambuliaji muhimu kwenye timu hiyo. Kwa muda mrefu hakuwepo kwenye timu ya taifa ya Uingereza kwa sababu ya kupata majeraha yaliyomfanya aweze kukaa nje wa muda mrefu.

Games 10

Games started 8

Mins played 673

Assists 1

Goals 6

Chances created 4

Goals/game 0.60

Win rate 50%

Danny Welbeck



Welbeck ni mmoja kati ya washambuliaji wenye uwezo mkubwa wa kurudi nyuma na kukaba wakati timu inashambuliwa. Japo amekuwa hayupo fiti kwa muda mrefu kutokana na kuwa nje ya uwanja kwa majeraha ya muda mrefu, kwa sasa Welbeck ameonekana kurudi na kuanza kufanya vizuri ingawa ameonekana hapati nafasi sana kwenye timu ya Arsenal.

Games 8

Games started 6

Mins played 501

Assists 2

Goals 3

Chances created 5

Goals/game 0.38

Win rate 38%

Andy Carroll



Kwa sasa Carroll ameonekana kuanza kurudi kwenye makali yake kama kipindi yupo timu ya Newcastle United kabla ya kuhamia Liverpool na kiwango chake kupotea. Hatrick yake kwenye mechi ya West Ham United dhidi ya Arsenal inamfanya Hodgson ajiulize mara mbili na kufikiria kuchanga karata yake vizuri.

Games 22

Games started 8

Mins played 1,010

Assists 1

Goals 8

Chances created 8

Goals/game 0.36

Win rate 41%

Marcus Rashford



Rashford amekuwa ni mmoja kati ya washambuliaji chipukizi wenye uwezo mkubwa wa kufunga magoli mazuri. Mpaka sasa Rashford ana umri wa miaka 18 ameonekana kuwa ni mmoja kati ya wachezaji tegemezi wa timu hiyo akiwa tayari kashafunga magoli 8 kwenye mashindano yote aliyoichezea timu ya Manchester United.

Games 7

Games started 7

Mins played 546

Assists1

Goals 4

Chances created 2

Goals/game 0.57

Win rate 71%


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment