Mamia ya watu jijini Dar es Saalam wamejitokeza kumzika msanii wa muziki wa dansi Ndanda Kosovo Kosovo aliyefariki dunia Jumamosi iliyopita katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Mama yake Ndanda akimuaga mwanae kwa mara ya mwisho
Mazishi hayo yamefanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar,na kuhudhuriwa na Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa Michezo, Mh Nape Moses Nnauye, Mkuu wa mkoa wa Kinondoni Paul Makonda, wasanii pamoja na wadau mbalimbali wa burudani.
Awali ya hayo, mwili wa marehemu Ndanda Kosovo, uliwasili ubalozi wa Kongo wa zamani, Kinondoni Ananasif ukitokea Muhimbili, ambapo ndugu wa marehemu, viongozi wa serikali pamoja na wasanii walipata fursa ya kuaga mwili kwa mara ya mwisho. Tazama picha.
Wadau waliyojitokeza kumzika Ndanda
Katibu Mkuu wa Basata, Geoffrey Mwingereza (katikati) akiwa kwenye mazishi
Mama yake Ndanda akimuaga mwanae kwa mara ya mwisho
Kuaga mwili wa marehemu
Lady Jaydee akisaini kitabu cha wageni
Mama yake Ndanda akimuaga mwanae kwa mara ya mwisho
Mama Yake Ndanda Kosovo akilia kwa uchungu
Nape akizungumza na Lady Jaydee baada ya kumaliza shughuli za kuaga mwili wa marehemu
Credit Bongo5
0 comments:
Post a Comment