Nimeshaenda sana kwa waganga lakini sikuona mabadiliko yoyote – Galatone


Msanii Galatone ameweka wazi kuwa alishawahi kwenda kwa wa Waganga wengi wa kienyeji ili afanikiwe kwenye sanaa ya muziki anayoifanya.



Akiongea katika kipindi cha Hatua Tatu cha Times Fm ijumaa iliyopita, Galatone amesema ilifika kipindi alichoka katika harakati za kuuhangaikia muziki ndipo ikamlazimu kuingia katika nguvu za giza.

“Nimefanya sana nimeenda kwa Waganga maana kuna kipindi nilichoka kabisa nkasema acha nikajaribu, nshavunja nazi, kuchinja kuku na kila kitu yani ili tu nitoboe kwenye game,” alisema.

Galatone amekiri kuwa hakupata chochote na wala hakuona mabadiliko yoyote ndipo akaamua kuachana na mambo hayo na kumtegemeea Mungu tu.

Credit Bongo5



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment