Yamoto Band na Kayumba wameandika wimbo ujao wa Shaa ‘Sawa’



Kundi la Yamoto Band pamoja na mshindi wa shindano la Bongo Star Search 2015, Kayumba, wameshirikiana kuandika wimbo ujao wa Shaa uitwao ‘Sawa.’



Shaa aliambia Bongo5 kuwa akiwa chini ya usimamizi wa Said Fella, amekuwa akikutana na vijana hao mara kwa mara kwenye studio za Mkubwa na Wanawe.

“Niko chini ya usimamizi wa Mkubwa na Wanawe kwahiyo nikifika pale wananiambia ‘dada Shaa tumekuandikia hii, hebu sikia.’ Nawasikilizaga kwasababu soko sasa hivi lipo kiujana zaidi, kwahiyo nikiona kwamba vijana wanajua soko liko wapi nawasikiliza,” aliongeza.

Video ya wimbo huo tayari imefanyika na kuongozwa na Justin Campus. Video na wimbo huo vitatoka hivi karibuni.

Credit bongo5

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment