Imani ni wimbo wa kuwapoza walioumizwa kimapenzi – Linah



Linah amesema wimbo wake mpya, Imani ni kwaajili ya kuwapoza wale walioumizwa kimapenzi.



Akiongea na Bongo5 Linah amesema, ” Unajua kila siku tunaimba furaha sana katika mapenzi, je tunawaangalia vipi wale ambao hawana furaha katika mapenzi? Nikaona niimbe wimbo ambao utawatia moyo katika mahusiano yao ambao huwa wanatengwa na familia. Unakuta wanaambiwa kuwa huyo mwanaume maskini, sijui mbaya, unakuta mwingine labda anaambiwa naye mwanamke wako mbaya. Kwa wimbo huu watu kama hao wakiusikiliza wanafarijika sana.”

Kuhusu kurudi kwenye muziki wa injili, Linah amesema, “Kwakweli sina uhakika kwa sasa kama Mungu atanibariki nitaweza au la maana ndio nilipoanzia huko kwahiyo sijajua huko mbeleni.”


Credit Bongo5.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment