Shilole aanzisha label ‘Shilole Entertainment’ amsaini msanii huyu



Msanii wa muziki Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameanzisha label yake mpya ‘Shilole Entertainment’ ambapo pia amemsaini msanii chipukizi aitwae ‘Amaselly’.


Shilole na msanii wake mpya aitwae Amaselly

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na video yake ya wimbo ‘SayMyName’, amekiambia kipindi cha Clouds E kinachoruka katika runinga ya Clouds TV, kuwa ameamua kuanzisha label hiyo ili kuwasaidia wasanii wenye vipaji lakini hawapati nafasi.

“Yeah nimemsani Amaselly aka Gaucho, kwa sababu ni msanii mwenye heshima, amenitafuta kwa muda mrefu, Shilole nisaidie nisaidie, kwa hiyo nikajifikiria, nikaamua kumsaidia,” alisema Shilole.


Shilole na Amaselly

Pia Shilole amesema amemsaini msanii huyo kupitia label yake mpya iitwayo Shilole Entertainment.

Kwa upande wa Amasely alimshukuru Shilole kwa uwamuzi wa kumsaidia huku akihaidi mambo mazuri.
Hii hapa chini ni moja kati ya kazi za msanii huyo ambayo aliifanya kipindi cha nyuma




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment