Real Madrid ya twaa kombe la klabu bingwa duniani


Klabu ya Real Madrid siku ya jumapili ya December 18, ilicheza dhidi ya Kashima Antlers ya Japani kwenye fainali ya FIFA Club World Cup.



Real ilipata goli lake la kwanza kunako dakika ya tisa kupitia mshambuliaji Karim Benzema, lakini Gaku Shibasaki alifunga mabao mawili katika kipindi cha kwanza na cha pili na kuiweka mbele Kashima.



Hadi dakika ya 90 mchezo uliisha kwa matokeo kuwa ni 2-2.

Mechi ikaelekea kwenye dakika za nyongeza na hapo ndipo Ronaldo akaamua mechi hiyo kwa kufunga hat-trick.

Baada ya filimbi ya mwisho Madrid ikawa mshindi kwa magoli 4-2.

Ushindi huo unaipatia Real Madrid kombe la pili la klabu bingwa dunia na kuendeleza rekodi yake ya kutoshindwa katika mechi zote hadi mechi 37.

Hatua hiyo ina maana kwamba washindi 10 wa taji hilo wanatoka bara Ulaya.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment