Video ya Mazoea imekula pesa nyingi sana – Billnass


Msanii wa muziki wa hip hop Billnass amedai uwekezaji mkubwa alioufanya kwenye video ya wimbo wake mpya ‘Mazoea’ ndio kitu ambacho kimeufanya wimbo huo kupokelewa kwa kasi zaidi.


Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa video ya wimbo huo ni moja kati ya video zake alizowekeza pesa nyingi zaidi.

“Mamshukuru mungu ‘Mazoea’ inaenda vizuri na tayari kuna simu za show ambazo nimeanza kupigiwa ili kurudisha kile tulichokiwekeza kwa sababu Mazoea ni moja kati ya video zangu ambayo imekula pesa nyingi sana,” alisema Billnass.

Bill amewashukuru mastaa mbalimbali pamoja na mashabiki wake ambao wameonyesha kuusupport wimbo huo aliomshirikisha rapper mkongwe, Mwana FA.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment