Yanga ilimaliza dakika 90 na KMKM ya Z’bar kwa Ushindi huu July 24 2015



Klabu ya Dar es Salaam Young African imezidi kujiweka kwenye nafasi nzuri katika michuano ya Kombe la KAGAME ambalo linaendelea Dar Es Salaam… Yanga ambayo ilianza mashindano hayo vibaya imeshacheza mechi tatu hadi sasa na kupoteza moja dhidi ya Gor Mahia ya Kenya ambayo iliwafunga goli 2-1.
Wachezaji-wa-Yanga-wakijadili-baada-ya-kufungwa-magoli-katika-kipindi-cha-pili.
July 24 2015 Yanga imetinga Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kucheza na KMKM ya Zanzibar ambapo Yanga imejiweka vizuri baada ya kuifunga KMKM ya Zanzibar kwa jumla ya goli 2-0, huu ni mchezo ambao umemfanya Malimi Busungu kuingia tena katika headlines baada ya kupachika goli la kwanza dakika ya 56 huku bao la pili KMKM wakijifunga wenyewe dakika ya 72.
yanga
Yanga ipo nafasi ya tatu katika kundi A kwa point 6 nyuma ya Al Khartoum ya Sudan na Gor Mahia ya Kenya, huku KMKM ya Zanzibar ikiwa nafasi ya nne na Telecom ya Djibout kushika mkia kwenye Kundi hilo.
Yanga-celebrate-300

YANGA II
YANGA
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment