Adebayor atemwa kwenye kikosi cha Tottenham


Emmanuel Adebayor ameachwa kwenye kikosi cha Tottenham Hotspur chenye wachezaji 25 kwaajili ya Premier League.



Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alitarajiwa kuondoka White Hart Lane lakini hakuna klabu iliyofikia makubaliano ya gharama za kumchukua.

Kutokana na hilo mchezaji huyo wa Togo ataendelea kupiga benchi Spurs hadi January pale ambapo atakuwa akifanya mazoezi na wachezaji wa ziada na timu ya vijana.

West Ham waliaminika kuwa mbioni kumsainisha kwa mkopo lakini walikuwa wameshafikia kikomo cha kuchukua wachezaji wa mkopo.

Hata hivyo mashabiki wengi wa Spurs wamekosoa uamuzi huo wakiamini kuwa ni bora angewekwa kwenye kikosi hicho hata kama angekuwa mchezaji wa ziada.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment