Danny Welbeck kukaa nje kwa muda mrefu
Mshambuliaji wa England na klabu ya Arsenal, Danny Welbeck hataonekana uwanjani kwa miezi kadhaa na anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa goti.
Ripoti iliyotoka kwenye mtandao wa klabu ya Arsenal inasema mshambuliaji huyo ambaye zamani alikuwa Manchester United amekuwa akitegemea kukwepa majeruhi na alishindwa kupona katika matibabu yaliyopita.
Kuwa majeruhi kwa Welbeck kutamuongezea presha kocha Arsene Wenger kufuatia kushindwa kumnasa Karim Benzema au Edinson Cavano kabla dirisha la usajili halijafungwa Jumanne.
0 comments:
Post a Comment