Baba yake na Beyonce agusia uwezekano wa ziara na album mpya ya Destiny’s Child


Ikiwa ni takriban miaka 10 tangu itoke album mpya ya Destiny’s Child, baba yake na Beyonce, Mathew Knowles amesema huenda kundi hilo likaungana kwa mara nyingine.



Akiongea na mtandao wa The Huffington Post, Knowles ambaye bado anasimamia kazi za kundi hilo alisema mashabiki watarajie kitu.

“Nina matumaini makubwa kuwa wasichana hawa watarejea na album na ziara. Ninafanyia kazi miradi michache ya Destiny’s Child kwa sasa,” alisema.

“Kitabu changu cha pili kitakuwa ni historia ya Destiny’s Child. Ninaongea na watu wa filamu na TV kwa sasa, kuhusiana na filamu ya Destiny’s Child au series, kitu kama hicho. Lakini bado nawasimamia wasichana hawa, na nina matumaini miaka miwili au mitatu ijayo tutaona makubwa kutoka kwao.”

Knowles amewahi pia kuwa meneja wa Beyonce.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment