Bobi Wine asema hana mpango wa kwenda kimataifa, anaridhika kuwa msanii wa ndani

Wakati wanamuziki wengine wa Afrika Mashariki wakiendelea kutafuta njia za kuvuka mipaka ili kutangaza muziki wao kimataifa, Bobi Wine kutoka Uganda amewashangaza wengi baada ya kusema kuwa anaridhika kuwa ‘local artist’ na hana mpango wa kwenda ‘International’.


Bobi-Wine

Akiongea kupitia kipindi cha The Beat cha NTV ya Uganda Ijumaa iliyopita, Bobi Wine amesema kuwa kazi yake ni kufanya muziki kwaajili ya mashabiki wake wa Uganda, na endapo mashabiki wa nje watapenda kazi hizo ni sawa, lakini haimaanishi kuwa ana mpango wa kufanya muziki kwaajili ya mashabiki wa nje.
Kauli hiyo inakuja kipindi ambacho mastaa wa Uganda kama Jose Chameleone, Bebe Cool, Eddy Kenzo na wengine wanafanya vizuri na kutajwa kuwania tuzo mbalimbali kubwa za kimataifa.





Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment